Robo Mwezi

Текст
0
Отзывы
Читать фрагмент
Отметить прочитанной
Как читать книгу после покупки
Шрифт:Меньше АаБольше Аа

"Safari ilikuwa aje?" akauliza Giulia.

“Vizuri sana, "ngombe huyo wa chuma" ina kasi sana na ina raha wakati unataka kusafiri; na jiji limejaa vitu vya kupendeza kuona. Ninafuraji kuwa hapa!"

"Tafadhali keti. Lazima umechoka. Je! Ungependa aiskrimu?" akauliza Giulia.

"Ndio, asante, Shangazi." Nimepokea kwa furaha Libero. "Wapi Elio?"

"Elio yuko katika chumba chake. Atakuwa hapa baada ya dakika chache." rakajibu Carlo. Alikuwa amekasirika kwa sababu mwanawe hakujisumbua hata kuja kusalimia binamu yake, ambaye amesafiri mwendo mrefu ili kumchukua. Alipoanza kutembea kuelekea kwenye chumba cha Elio,

Libero alianza kuongea:"Usijali, mjomba Carlo. Nitaenda. Nataka kumshangaza. Niambie tu chumba chake ni kipi."

Mara tu Carlo alipomwonesha chmba cha Elio, Libero akamka kuelekea mlangoni. Kilio cha furaha cha Libero kilisikika kwenye ushoroba wakati alipokuwa akimsalimia binamu yake.

Hata Elio, licha ya utulivu wake hakuweza kuepuka kukumbatiwa na Libero.

Gaia alimtazama mamaye na kunong'ona:

"Sikukumbuka kwamba alikuwa anaweza kudanganywa hivyo!"

"Usiseme hivyo." Maramoja akamkaripia Giulia. "Ni mvulana mzuri. Na ni mwema sana pia."

"Ndio, lakini... Unauhakika atatuendesha salama hadi tufike shambani." Bila shaka aliuzila Gaia.

"Kweli, hiyo atafanya!" akamtuliza Carlo. "Usimdharau. Yeye na mama yake anaendeleza kazi ya shambani. Yeye ana nguvu na ni mwerevu."

Wakati wa chakula cha jioni ulifika na kuendelea kwa furaha. Kwa kweli, Libero alikuwa amemletea sherehe zote na uchangamfu wa vijijini, ambayo ilithaminiwa san ana kila mtu isipokuwa Elio.

"Nasubiri sana kukuonesha huku." Alimaliza Libero baada ya kueleza mambo ya shamba kwa binamu yake.

"Una uhakika kwamba hutaki kukaa kwa siku kadhaa kabla ya kuondoka tena?" akauliza Giulia.

"Siwezi kumwacha mama pekee yake wakati huu wa mwaka. Kuna mambo mengi ya kufanya."

"Uko sahihi, Libero. Kwa kweli wewe ni mvulana mzuri." akamsifu Carlo, akimpapasa kwa upole begani.

"Unajua, mjomba Carlo, nilikuwa najiuliza kitu. Kabla ya kuja huku mjini, nilifikiria unatakiwa kupiga honi tu wakati wa dharura...."

"Ndio, hiyo ni kweli." akajibu Carlo. "Kwanini?"

"Kwa sababu inaonekana kila mtu hutumia kana kwamba walikuwa wanacheza muziki kwenye sherehe! Hawaachi kupiga honi!"

Kila mtu aliangua kichezo, isipokuwa Elio, ambaye alijiuliza iwapo Libero alikuwa akitania au la ...

Sura ya tatu

Aligundua kuwa mvulana huyo alikuwa ametishika, na akaangua kicheko

Asubuhi ya siku iliyofuata Libero alimtoa Giulia kwenye kitanda chake baada ya kujikwa kwenye zulia la ushoroba. Kwa hivyo, Giulia na yeye walijikuta wakila kiamsha kinywa kabla ya kila mtu kuamka. Wakati harufu ya kahawa safi ilipokuwa iliovamia chumba cha kulala cha Carlo, pia alielekea jikoni na kuanza kuelezea kile kilichokuwa kimemekabili Elio siku za hivi karibuni.

"Usijali." aliwahakikishia Libero. "Uzoefu huu wa nje utamsaidia. Na mama tayari ana mkakati! "

Mara tu walipofika kituo cha gari moshi, Giulia hakuweza kuacha kutoa mapendekezo na kuhakikisha kuwa watoto watakuwa na tabia nzuri.

Gaia hakuweza kusubiri; alikuwa amesisimika na mdadisi. Kwa upande mwingine, ilikuwa wazi kwamba Elio alikuwa akiburuzwa tu kwenye hayo. Zaidi ya hayo, pia alikuwa amebeba mizigo mizito ya Gaia kwa sababu tu Libero alimfanya kufanya hivyo: "Wanawake hawapaswi kubeba uzito!" alisema, ambayo ilisababisha Elio atumbue macho. Hakuweza kumvumilia binamu yake tayari.

Libero alikuwa amevaa suruali ya khaki, t-shati na kofia ya kujikinga ya baseball ya manjano, ambayo ilionekana isiyofaa kabisa kwa binamu zake. Zaidi ya hayo, alikuwa amebeba mizigo iliyobaki kwa wepesi kiasi kwamba inaweza ilikuwa haina kitu ndani.

Treni iliondoka kwa wakati ufaao. Hakuna mtu mwengine aliyekuwa ndani ya gari walilokuwa wametengewa. Baada ya Libero kupanga mizigo yote kwenye juu ya gari, alipendekeza:

"Gaia, andamana nami. Hebu tuende kwenye mgahawa wa gari na tupate kiamsha kinywa zaidi. Itakuwa safari ndefu na utahitaji nguvu zako zote. Elio anaweza kuchunga mizigo. Hata hakuna mtu atakayeikaribia. Ikiwa mtu atagusa, bweka! " alisema Libero kwa binamu yake. "Na ukiacha kukasirika, tunaweza hata kukuletea chakula..."

Gaia na Libero walitoka nje ya gari, na kumpa Elio faraja kubwa kwa kuwa alitaka kuwa peke yake.

Alikuwa akiangalia mandhari ya nje kupitia dirisha lake. Walikuwa wamesafiri kupita eneo la viwanda la jiji na walikuwa wameanza kuzungukwa na mashamba na milima ambayo ilikuwa ikibadilishana tena na tena.

Ghafla, kwenye kidirisha cha dirisha akaona sura ya mzee amekaa kwenye kiti cha kando kiti chake.

Aliingia lini kwenye gari? Hakusikia milango ikifunguliwa.

Mzee huyo alikuwa amevaa nguo nyeusi na alikuwa amevaa miwani isiyo ya kawaida puani. Alikuwa akisoma kitabu cheusi cha ngozi ambacho kilionekana kama cha karne moja kilichopita, ambacho kurasa zake zilitengenezwa kwa karatasi ya tishu. Kichwani alikuwa na kofia yenye kuta pana iliyokuwa inaficha uso wake. Mandhari yote ilikuwa isiyo ya kutuliza.

Elio hakugeuka, lakini alikuwa akimwangalia kupitia akisi kwenye kidirisha cha dirisha. Alihisi kuogopa kuwa peke yake na mtu huyo. Wakati huo kwa hakika alitaka binamu yake mkubwa na mwenye nguvu awe karibu naye. Walakini, yeye wala Gaia hawakuwa wakionekana.

Wakati uuo huo, mzee huyo alikuwa bado anasoma kitabu chake. Kila baada ya muda, angeangalia saa ya zamani ambayo alikuwa akiiweka ndani ya mfuko ulio kwenye kifua cha koti lake la kiuno, alilokuwa amevaa kwa maridadi ndani ya suti yake ya zamani.

Hii ilimkera Elio zaidi, ambaye aliendelea kujiuliza huyo mtu anangojea nini au nani. Hakika lazima ilikuwa ni kitu cha umuhimu wa ajabu kutokana na jinsi alivyokuwa akiangalia saa yake kila wakati.

Ghafla, baada ya kuangalia saa tena, yule mzee alifunga kitabu chake na kuinama ili kutoa kitu ndani ya begi jeusi alilokuwa akiiweka katikati ya miguu yake. Alipokuwa akiinama chini, suruali yake ilipanda juu kidogo na kufunua vifundoni vyake vyeusi na soksi fulani nyembamba nyeusi ambazo zilionekana kama manyoya nyeusi.

Elio hakuweza kuzuia hofu yake na akaanza kutetemeka. Alipokuwa akiangalia ndani ya begi lake mwenyewe,mzee huyo akaangua kicheko kana kwamba alitambua hofu ya Elio. Kilikuwa kicheko kirefu, cha kina na cha huzuni ambacho kilisikika masikioni mwake. Elio aliziba masikio yake kwa mikono kujaribu kuzuia kusikia kelele hizo. Alifunga macho yake ili kuepuka kutazama akisi ya mtu huyo kwenye kidirisha cha dirisha na kuanza kusali: "Libero, rudi. Libero, rudi. "

Kisha, mlango wa gari unaotumia mtambo ulifunguliwa ghafla.

"Elio, unafanya nini? Je! Ulipata maambukizi ya sikio jijini? Usituambukize sisi wananchi na virusi hivyo vya mijini! "

Elio alishtuka. Halafu, baada ya kutambua sauti changamfu ya Libero, aligeuka nyuma na kumwona binamu yake akicheka; alikuwa ameshika begi lililokuwa na bidhaa alizonunua na kinywaji laini mikononi mwake. Gaia alikuwa amesimama nyuma yake na alikuwa akiuma kwa mkoromo kubwa.

Hakukuwa na dalili ya mzee huyo. Alipotea tu jinsi alivyokuwa ameonekana hapo awali. Kila kitu chake kilipotea: kitabu chake, saa yake na begi lake.

Libero aliketi karibu na Elio na baada ya kumpa mkoromo, aligundua alikuwa akitetemeka.

"Kuna kitu kilitokea?" Aliuliza.

"Nadhani ni ugonjwa wa mwendo tu." alidanganya Elio.

Gaia alielewa kuwa kaka yake alikuwa na shida moja na akaahidi mwenyewe atashughulikia shida hiyo kwa Libero.

Safari iliyokuwa imesalia ilikuwa ya utulivu. Libero alielezea tamasha la mavuno ambalo lingefanyiwa hivi karibuni na litahusisha vijiji vyote jirani. Litafanywa nje na jioni watachangamshwa na densi za kitamaduni kama taranta, na nyingine za kisasa.

Elio alikuwa akimwangalia dada yake na binamu yake, na akajiuliza ni vipi hawa wawili wameweza kuelewana haraka sana. Licha ya hayo, alifurahi kusafiri nao. Matukio yote hayo yalikuwa yakimpa wasiwasi. Alikuwa akiathiriwa na aina fulani ya njama dhidi ya hisia zake, au alikuwa akienda mwendawazimu?

Libero aliingiwa na woga kwani ilikuwa wakati wa kushuka kwenye gari moshi. Aliona kupitia kwenye dirisha nyumba ya Bibi Gina, ambayo ilichukuliwa kama sehemu ya kumbukumbu. Mara tu gari moshi liliposimama, akachukua mifuko. Halafu, baada ya Gaia kufungua mlango, kwa woga alitoka nje ya gari moshi kama wale ambao hawajazoea kusafiri mara nyingi.

Wenyeji wangechukulia sehemu hiyo kama kituo cha reli, lakini kwa kweli haikuwa chochote isipokuwa mahali tu pa kusimama katikati ya mahali pasipojulikana. Starehe pekee walizopewa na paa la jukwaa lililobomoka na mashine ya tikiti iliyovunjika ambayo ingeweza kupitisha ujumbe uliokwisha kurekodiwa ukisema "Uwe mwangalifu, kituo hiki hakiangaliwi. Jihadharini na wezi wa mfukoni ".

Libero akachukua pumzi nzito na kusema:

"Hatimaye, hewa safi. Karibu Campoverde. "

"Tayari ninahisi harufu ya mashamba." aligundua Gaia. "Unaweza, Elio?"

Elio hakuweza kuhisi tofauti yoyote ikilinganishwa na jiji, na alinyanyua mabega yake tu.

"Elio, chukua mzigo wa Gaia. Nitabeba hizo nyingine. "Akaamuru Libero.

Gaia bila kutarajia alifurahia tabia ya kiungwana ya Libero, ambayo kawaida ingemkasirisha. Lakini Libero alikuwa mkweli sana hivi kwamba alifurahishwa nayo na alikubaliana naye. Labda alikuwa na haraka ya kumchukulia kama mpumbavu...

Gaia na Libero walitembea mbele ya mashine ya tiketi ya kuzungumza, ambayo ilikuwa ikirudia rudia sentensi, na kisha wakaelekea upande wa chini wakitabasamu.

 

Ilibidi Elio anyakue mzigo mkubwa wa Gaia kwa mpini wake ili kushuka chini na kupanda ngazi za tombwe. Alikuwa amechoka kabisa.

Katika hatua chache za mwisho alifanya juhudi za mwisho akitumaini kwamba shangazi Ida angekuwa akingojea katika maegesho ya gari kuwapeleka nyumbani.

Lakini alipoingia kwenye maegesho, aligundua kuwa hakuna mtu aliyekuwa akiwasubiri. Libero, akiwa na Gaia kando yake, wakaelekea magharibi kwa kuambaa barabara nyembamba ambayo ilikuwa na lami duni. Mifereji miwili ilikuwa ikitiririka kando ya barabara na ilikuwa ikiitenganisha na mashamba ya mahindi upande mmoja na mashamba ya ngano upande mwingine.

Elio, ambaye alikuwa akihema, aliwapigia kelele kusimama kwa sekunde moja. Dada yake aligeuka akiwa amechanganyikiwa. Hangeweza kukumbuka mara ya mwisho kaka yake alizungumza kwa sauti kama hiyo, wala kupiga kelele namna hiyo.

"Gari la shangazi Ida liko wapi?" aliuliza Elio.

"Ah, samahani nimesahau kukuambia. Alinipigia simu akisema kwamba hawezi kuja. Camilla, ng'ombe wetu, yuko karibu kuzaa na mama hawezi kumwacha peke yake kwa sasa. "

"Camilla? Karibu kuzaa? Tutafanya nini? " Elio aliuliza akihema.

''Usiwe na wasiwasi. Ni maili nne tu na tutakuwa shambani. "Alijibu Libero kwa utulivu.

"Maili nne?" yalikuwa maneno ya mwisho ya Elio.

"Huamini! Mizigo ya dada yako ni ya kubeba! " alimtania Libero, kisha akarudi kutembea.

Kwa mbali nyumba kadhaa za kwanza zinaweza kuonekana.

"Ndio hapa! Nyumba ile nyuma ya mti wa cheri ni yetu. Ni shamba. "

Libero alionesha shamba jekundu la veneti lililo na mimea.

Bustani nzuri na iliyotunzwa vizuri iliyonyooka kutoka mlango wa mbele hadi laini za kuanikia nguo zilioaashiria mwanzo wa zizi. Zaidi ya hapo ni mashamba tu yake.

"Mama, tuko hapa!" alipiga kelele Libero, akiacha mizigo barabarani na kukimbia kuelekea zizi.

Shangazi Ida alitoka nje kupitia mlango wa mbele.

"Mpwa wangu wa kiume na wa kike!" alipiga kelele kwa furaha.

Gaia aliweka mikono yake shingoni mwake. Elio, ambaye alikuwa amechoka, alimsogelea na kumpiga busu shavuni. Nikuwe tu na heshima.

Ida alikuwa mtu mwenye umri zaidi ya miaka 50, lakini urembo wake wa asili ulikuwa haujafifia bado. Alikuwa mwanamke mwembamba, mwenye urefu wa wastani... Mwili wake ulikuwa uliwiana vizuri ingawa, mikono na miguu yake ilikuwa ya misuli na nguvu kuliko ya mwanariadha. Maisha magumu ya shamba ilikuwa mazoezi yake ya mwili ya kila siku. Alikuwa na nywele nyeupe zilizofungwa kama mkia wa farasi, na ngozi yake nzuri ingemfanya macho yake mazuri ya kijani kuonekana, kama ya mpwa wake.

Wakati huo huo, Libero alikuwa akirudi kutoka kwenye zizi, wote wakitabasamu.

"Camilla alizaa ndama wa kike! Maziwa zaidi kwetu! "

Shangazi Ida aliwaalika ndani ya nyumba. Meza iliandaliwa na harufu ya chakula kitamu cha mchana ilikuwa ikielea hewani. Watoto walikuwa na njaa na walikula vyakula vyote. Gaia hakuweza kuacha kumwambia shangazi yake hisia zake ambazo alikuwa amehisi wakati wote wa safari.

Baada ya chakula cha mchana, Gaia alimsaidia Ida kusafisha vyombo. Libero, kwa upande mwingine, alimburuta Elio kwenda shambani akimuuliza, au tuseme akiamuru amsaidie.

Wakati wa jioni, shangazi Ida alielezea kuwa chumba kilichoko darini kitakuwa chumba chao cha kulala cha majira ya joto. Walakini, kwa sasa walikuwa wakilala kwenye kitanda cha sofa sebuleni hadi chumba cha kulala darini kitapokuwa tayari.

Gaia alipanda juu ghorofani na kumfuata shangazi yake kuona chumba cha darini. Kwa upande mwingine, Elio alishtushwa na habari hizo mbaya za ziada.

Walikwenda juu hadi ghorofa ya kwanza, ambapo Ida na Libero watakuwa wakilala. Kwenye ghorofa iyo hiyo, pia kulikuwa na chumba cha kulala cha Ercole, binamu yake mdogo kabisa ambaye alikuwa amekwenda kwa kambi ya majira ya joto. Ida alionesha ngazi ya mbao iliyokuwa ikielekea kwenye dari. Hatapanda pale kwani tayari alikuwa amechoka kwenda juu na kurudi chini kwa ngazi. Kwa kweli, alikuwa tayari kwenye chumba hicho wakati wa mchana ili asafishe chumba hicho.

Wakati uo huo, shangazi Ida aliingia chumbani kwake na kwa siri alimwita Giulia, shemeji yake, ili amsasishe.

Simu haikulia hata mara mbili. Giulia alichukua mara moja.

"Habari mpenzi, unaendeleaje?" aliuliza Ida.

"Kila kitu kinaendelea vizuri, asante. Lakini niambie. Aliendaje? "

"Aliweza kutembea hadi hapa kutoka kituoni bila kuchoka. Alifikiri nitawapeleka nyumbani kwa gari. Libero alidanganya na kumwambia kwamba ng'ombe wetu, Camilla, alikuwa anakaribia kuzaa. "Akacheka Ida.

"Ningetaka kumuona akitokwa na jasho!"

"Baada ya kula chakula cha mchana ..." alianza kusema Ida, lakini Giulia akamkatisha.

"Je! Alikula chochote?"

"Ndio, alikula mara mbili."

Loo! Nyumbani hakuli hata mkate wa sandwichi. "

"Ni ngumu hata kama." Alisema Ida. "Lakini nina uhakika atakuwa sawa."

Kwenye usuli aliweza kusikia Carlo akiuliza maswali na kucheka.

"Michezo ya Runinga na video hakuna. Katika msimamo mkali wa mwisho. "

Elio, ambaye alikuwa amelala kitandani. Hakuweza kusogeza mwili wake. Ilikuwa imepita miaka kadhaa tangu atembee kiasi hicho.

Shuleni kila wakati alikuwa akitoa visingizio ili kuepuka darasa la mazoezi.

"Elio mwite dada yako hapa. Ninahitaji usaidi wa chakula cha jioni. "

Elio hakuamini kile alichokuwa amesikia. Hakuweza kuwa kwa kweli.

Lakini shangazi Ida aliongea kwa sauti ambayo haingeruhusu jibu lolote hasi.

"Elio, umesikia nilichosema?"

"Sawa." alijibu na kuendelea kuelekea ngazi ya ghorofa akiwa na uso zote mkali.

Alisimama chini ya ngazi ya mbao na kuanza kupiga kelele akiita jina lake.

Licha ya kelele za kaka yake, Gaia hakuwa akijibu.

Ndipo Elio, akiwa amekasirika zaidi, aliamua kupanda ngazi. Katika chumba cha dari kilichokuwa na giza alikuwa akihisi wasiwasi. Hatua kwa hatua, safari ya dari ilionekana kuwa haina mwisho. Punde tu alipofika na kichwa chake chini ya sehemu iliyoanguliwa, alianza kupiga kelele akiita jina la dada yake. Lakini tena, hakuna aliyejibu. Alijilazimisha kutembea hatua za mwisho. Na kisha kitu kutoka juu kilishika mkono wake.

Elio alikaa kimya, macho yake akiwa ameyafumba na sura ya kutishika usoni mwake.

"Unayo!" alipiga kelele Gaia, ambaye alikuwa amegundua kuwa Elio alikuwa na hofu.

"Ondoka kwangu. Umeniogopesha. Ungejibu. "

Gaia hakukubali hayo kwani alikuwa akivutiwa na kile alichokuwa amefahamu, na akasema:

"Dari hii imejaa vitu visivyo vya kawaida. Njoo hapa. Tazama hii..."

Elio alimaliza kupanda ngazi na kumfuata dada yake, ambaye alikuwa akivinjari picha za zamani.

"Hii ni ya kuchekesha." Alisema, akipitisha picha kwa Elio.

"Ni nini cha kuchekesha?" aliuliza Elio.

"Nini?" aliuliza Gaia. "Je! Humtambui?"

"Nani?!" aliuliza tena Elio.

"Ni baba!" alishangaa Gaia.

"Baba? Umesema kweli. Sikumtambui akiwa amevaa hivi. Anaonekana kama Libero. Wamevaa nguo zinazofana! "

Hatimaye, baada ya muda mrefu sana, alitabasamu. Wakati huo huo, Gaia, aliendelea kutazama picha nyingine.

"Umeiona hii? Nadhani ni Libero akiwa mchanga sana. Anaonekana kuwa sura nzito sana na mwenye huzuni hivi kwamba haionekani kama ni yeye. "

Picha hiyo ilionesha mtoto aliyeparara na dhaifu na mwenye amekaza macho.

"Anaonekana kutengwa sana" akasema Gaia.

Katika picha hiyo, alikuwa amesimama kwenye bustani na alikuwa ameshikilia mikononi mwake magari yake ya kuchezea. Picha hiyo ilikuwa imechukuliwa jioni na jua likiwa linatua nyuma yake. Libero alikuwa peke yake kwenye picha, hata hivyo kulikuwa na kivuli cha pili kando yake.

Elio aliiona na kwa wasiwasi akasema:

"Je! Unaweza kuona kivuli hiki?"

"Gani?"

Elio alianza kuhisi uwoga.

"Hii hapa. Huioni? Kivuli hiki haihusiani na chochote "alisema, akionesha picha hiyo kwa kidole chake.

"Hii? Ni kivuli cha mti. "

Gaia pia hakuamini, lakini alijaribu kumtuliza kaka yake.

Elio hakutaka dada yake afikirie kuwa alikuwa amerukwa na akili, na akaamua kubadili mada ya majadiliano.

"Lazima tushuke chini. Shangazi Ida amenifanya nije hapa nikuite. Anahitaji msaada wako. "

"Unakaa humu ndani?" aliuliza Gaia akiwa anaruka kuelekea kwa ngazi.

Elio alifikiria kwamba hakukuwa na nafasi kwamba angekaa hapo peke yake.

"Hapana, naenda na wewe" alijibu.

Gaia alimkuta shangazi yake akiwa na kazi ya kuandaa chakula cha jioni na akaanza kumsaidia.

Elio alikuwa karibu kulala katika sofa aliposikia sauti ya Ida.

Je, unafanya nini? Njoo utusaidie. Sio wakati wa kupumzika. Andaa meza, tafadhali.

"Libero yuko wapi?" aliuliza Gaia.

"Hakika anafunga zizi." alijibu Ida. "Elio, ikiwa umemaliza, unaweza kwenda kumwita hapa?"

"Nitaenda." alijitolea Gaia akitabasamu.

"Hapana, nakuhitaji hapa. Mwache ndugu yako aende."

"Ndio." kwa uchovu alijibu Elio, ambaye alikuwa na njaa isiyo ya kawaida.

Alitoka nje ya mlango wa mbele na kumtafuta binamu yake, ambaye alikuwa amekaa kwenye trekta uwanjani, akiangalia angani.

Elio alimwendea na alikuwa na hisia kwamba kila mtu katika familia hiyo alikuwa amekuwa kiziwi: alimwita mara kadhaa, lakini Libero hakujibu.

"Natumai kweli inaambukiza. Angalau nitaweza kujilaza na sitahitaji kusikiliza maagizo ya mtu yeyote. "Alitafakari Elio.

Yeye ilibidi atembee chini ya trekta ili apate jibu.

"Kwanini unapiga kelele?" aliuliza Libero.

"Unapaswa kuingia ndani. Chakula cha jioni tayari "alijibu Elio.

"Njoo juu." Alisema Libero, kana kwamba hakusikia maneno yoyote aliyokuwa akisema Elio.

"Huko juu?"

"Ndio, juu hapa. Nitakuonyesha kitu. "

Elio akapanda juu ya trekta na kuketi karibu naye.

"Angalia jinsi ilivyo nzuri." Alishangaa Libero, akiashiria angani. "Miaka michache iliyopita sikuweza kuiona."

"Nini?" aliuliza Elio huku akijaribu kugundua kile alikuwa akimaanisha.

"Anga." akarudia.

"Anga?"

"Ndio, anga. Ni jambo zuri. Lakini mara nyingi katika maisha yetu hatuinui vichwa vyetu. Wala simaanishi kuangalia hali ya hewa tu, lakini kuifikiria, kwa kimya, kwa njia ile ile tunayofikiria bahari. Ni vile tu ni rahisi kupenda bahari; ndiyo sababu inathaminiwa mara nyingi. Je! Umewahi kusimama na kupendezwa na anga? "

"Hapana."

Unapaswa: Inakuinua na kukufanya uangalie mambo kwa mtazamo sahihi. "

Elio, akishangazwa na akili ya binamu yake, alikaa kimya pamoja naye na akatazama angani kwa muda.

Kutoka weupe wa theluji hadi kijivu cha moshi, mawingu yalikuwa yakielea kati ya vipande viwili vya anga. Ukanda uliokuwa chini yao ulikuwa na kijivu cha risasi, ukanda uliokuwa juu yao ulikuwa wa samawati, uliangazwa na miale ya mwisho ya jua iliyokuwa ikitua. Ukingo wa mawingu ulionekana dhahabu, kana kwamba uliangazwa na nuru ya ulimwengu mwingine, kana kwamba yalikuwepo kuangazia maisha ya zamani. Nyeupe zilikuwa nene kama vilele vikali, zile za kijivu zilikunjana kama mchoro wa mtoto.

Kati yao, moja inaweza kutofautishwa kwa urahisi. Ilikuwa na umbo la nyati na ilikuwa imesimama dhidi ya usuli nyeupe kana kwamba mnyama wa kijivu alikuwa akikimbia kwenye milima nyeupe ya mbinguni. Kama fresco iliyochorwa na Tiepolo1, paa la asili lisilo na mwisho lilikuwa limenyooshwa juu ya kile kinachoonekana, juu ya siri ya uwepo wa roho zetu: ndogo sana, lakini ya milele.

Ghafla, Libero akaruka chini.

"Nimekufa na njaa sasa" alisema, akicheka sana.

"Na wewe, Elio?"

"Ndio."

"Haya, twende tukala. Labda wakati mwingine nitakuendesha tuzunguke na trekta. "

Alisema, akielekea nyumbani kwake.

Elio hakupoteza muda akaanza kumfuata. Alikuwa na njaa pia.

Купите 3 книги одновременно и выберите четвёртую в подарок!

Чтобы воспользоваться акцией, добавьте нужные книги в корзину. Сделать это можно на странице каждой книги, либо в общем списке:

  1. Нажмите на многоточие
    рядом с книгой
  2. Выберите пункт
    «Добавить в корзину»